Pages

Tuesday, December 26, 2017

Kazi kwako mdau wangu.........Tetesi za soka Ulaya 26.12.2017.




Kocha wa Man United Jose MourinhoManchester City inakaribia kumsajili kwa dau la £60m beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26. (Telegraph)
Mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho analenga kumsajili kiungo wa kati wa Argentina Paulo Dybala, 24, katika dau la £60m kutoka Juventus. (Daily Star)
Wakati huohuo manchester United imeimarisha dau lake kwa kiungo wa kati Marouane Fellaini, ili kumzuia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 ambaye I yake inakamilika mwishoni mwa msimu huu (Daily Express)

United pia imeanza mazungumzo na mshambuliaji wa Bordeaux ,20, Malcom, huku mkufunzi Jose Mourinho akiajindaa ku;ipa dau la £33m. (Daily Mail)
Arsenal wameambia kwamba ni lazima walipe dau la £40m kumsajili mshambuliaji wa Ujerumani Julian Draxler, 24, kutoka Paris St-Germain. (Mirror)

The Gunners wako katika ushindani mkali na Liverpool wa kutaka kumsajili mshambuliaji wa PSV Eindhoven Hirving Lozano mwenye umri wa miaka 22, ambaye ana thamani ya £42m. (Daily Star)
Hatahivyo usajili wa mchezaji huyo wa hadi £35m utaifanya Arsenal kumuuza mshambuliaji wake Alexis Sanchez, 29, mnamo mwezi Januari. (Daily Mail)

Mkufunzi Antonio Conte ameitaka usimamizi wa Chelsea kuwasajili wachezaji watatu wapya mnamo mwezi Januari. (Mirror)
Mkufunzi mpya wa West Ham David Moyes ana hamu ya kumsajili Steven Nzonzi iwapo Sevilla itaamua kumuuza mchezaji huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 29 mwaka ujao. (Guardian)

Celtic Imekana madai kwamba imekubali ombi la £18m kumuuza mshambuliaji Moussa Dembele, 21, kutoka . (Sun)
Mkufunzi Roy Hodgson anahofia kwamba Crystal Palace italazimika kumuuza Wilfried Zaha mwezi ujao huku Manchester City, Chelsea na Tottenham zote zikimtaka winga huyo ,25, (mirror)

Uingereza inatarajiwa kucheza mechi ya kujiandaa katika uwanja wa Leeds huku meneja Gareth Southgate akataka kuungwa mkono kabla ya michunao ya kombe la dunia ya 2018 nchini Urusi.(Times, subscription required)
Mkufunzi wa Everton Sam Allardyce amefichua kwamba aliisaidia kuimarisha motisha ya mabeki Michael Keane na Ashley Williams kupitia usaidizi wa mchezo wa runinga wa The Cube. (Liverpool Echo)

No comments:

Post a Comment