Pages

Monday, January 1, 2018

Moto wateketeza magari 1,400

Moto mkubwa umeharibu karibu magari 1,400 kwenye jengo la ghorofa la kuegesha magari huko Liverpool na kuwalazimu watu wengi kuukaribisha mwaka kwenye makao ya muda.

Wazima moto walisema kuwa moto huo katika jengo la King's Dock karibu na ukumbi wa Liverpool Echo Arena, ni mioto mibaya zaidi kuwai kukabiliana nayo

Polisi walisema uchunguzi wa awali ulionyesha kuwa moto kutoka kwa gari ulisambaa kwenda kwa mengine.

Watu walihamishwa kutoka majengo yalito karibu kutokana na moshi.

Polisi wa Merseyside walisema kuwa magari ya kuzima moto 21 yalikuwa eneo hilo na huma za wazima moto zilesema zilikuwa zinachukua tahadhari ya jengo hilo kuporomoka.

Magari yote yaliyokuwa kwenye jengo hilo linaloweza kuegeshwa magari 1600 yaliharibiwa. kwa mujibu wa polisi.

Waliwashauri watu kubaki manyumbani mwao na kufunga madirisha ikiwa wangeona moshi kutoka kwa moto huo.

No comments:

Post a Comment